1 Peter 1:10-12

10 aKwa habari ya wokovu huu, wale manabii waliosema kuhusu neema ambayo ingewajia ninyi, walitafuta kwa bidii na kwa uangalifu mkubwa, 11 bwakijaribu kujua ni wakati upi na katika mazingira gani ambayo Roho wa Al-Masihi aliyekuwa ndani yao alionyesha, alipotabiri kuhusu mateso ya Al-Masihi na utukufu ule ambao ungefuata. 12 cWalidhihirishiwa kwamba walikuwa hawajihudumii wao wenyewe, bali waliwahudumia ninyi, waliponena kuhusu mambo hayo, ambayo sasa yamehubiriwa kwenu na wale waliowahubiria ninyi Injili kwa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. Hata malaika wanatamani kuyafahamu mambo haya.

Mwito Wa Kuishi Maisha Matakatifu

Copyright information for SwhKC